Shambulizi la makombora la Urusi kaskazini mwa Ukraine laua watu 14

 

Shambulizi la kombora la Urusi limeua watu 13 katika mji wa Chernihiv kaskazini mwa Ukraine, kulingana na maafisa wa Ukraine.

Waziri wa mambo ya ndani wa Ukraine amesema kuwa kuna zaidi ya watu 60 waliojeruhiwa katika shambulizi hilo lililokumba jengo la orofa nane katika eneo lenye watu wengi.

Makombora matatu yalishambulia karibu na katikati mwa jiji, maafisa walisema.

Shambulio hilo lilitokea saa chache baada ya ripoti za shambulizi la Ukraine kwenye uwanja wa ndege wa jeshi la Urusi huko Crimea inayokaliwa.

Maelezo bado hayajathibitishwa, ingawa vituo vya mitandao ya kijamii vilishirikisha video ya moto unaoonekana kwenye uwanja wa ndege huko Dzhankoy kaskazini mwa Crimea.

Huko Chernihiv, kaimu meya Oleksandr Lomako alisema jengo moja lilikumbwa na mlipuko wa moja kwa moja kutoka kwa moja ya makombora ya Urusi na ghorofa kadhaa zimeharibiwa.

Ofisi ya rais mjini Kyiv ilisema majengo mengine manne ya juu, hospitali, makumi ya magari na taasisi ya elimu ya juu yote yameharibiwa katika shambulio hilo.

Waziri wa Mambo ya Ndani wa Ukraine Ihor Klymenko alisema kuwa watoto wawili walikuwa miongoni mwa waliopoteza maisha, na polisi walikuwa wakitafuta vifusi kwa waathiriwa zaidi.

BBC

No comments