Hatua zilizochukuliwa na Saudi Arabia katika Hijja ya mwaka huu

 

Zaidi ya Waislamu milioni 1.4 wanatekeleza ibada ya Hija katika mji mtakatifu wa Mecca nchini Saudi Arabia mwaka huu, baada ya mwaka mmoja ambapo watu 1,300 walifariki, wengi wao kutokana na joto kali.

Mamlaka za Saudia zilisema zimeongeza tahadhari za usalama kwa mahujaji. Wamepanda maelfu ya miti na kuweka mamia ya viyoyozi katika sehemu mbali mbali za ibada ili kusaidia kupunguza halijoto kali huko.

Serikali ya Saudi Arabia pia imeweka marufuku ya kupeleka watoto walio chini ya umri wa miaka 12 na kuonya kuwa watu watakaojaribu kuhiji kinyume cha sheria bila kibali rasmi watakabiliwa na faini ya dola 5,000 na kupigwa marufuku kwa miaka 10 kuingia Saudi Arabia.

No comments