Mvua kubwa yasababisha mafuriko huko Dubai

 

Mvua kubwa imenyesha katika maeneo ya Ghuba na kusababisha mafuriko ambayo yamesababisha vifo vya watu 20 na kutatiza safari za ndege katika uwanja wa ndege wa pili wenye shughuli nyingi zaidi duniani.

Uwanja wa ndege wa Dubai ulisema ulikuwa unakabiliwa na "wakati mgumu sana" siku ya Jumatano. Ilishauri abiria wasijitokeze kwani njia za kupaa kwa ndege zilikuwa zimejaa maji.

Kaskazini zaidi, mwanamume mmoja alifariki baada ya gari lake kukabiliana na mafuriko.

Huko Oman, waokoaji walipata mwili wa msichana huko Saham, na kufanya idadi ya vifo nchini kufikia 19 tangu Jumapili.

Mamlaka pia ilionya kuwa mvua nyingi zaidi za radi, mvua kubwa na upepo mkali zilitabiriwa, huku maeneo mengi ya mabondeni yakiwa bado chini ya maji.

Zaidi ya watu 1,400 wamehamishwa hadi kwenye makazi salama. Shule na ofisi za serikali zimefungwa kama tahadhari.

UAE inajulikana kwa hali ya hewa ya joto na jua, ingawa mvua kubwa imekuwa ya kawaida katika miaka ya hivi karibuni.

BBC

No comments