TANZANIA NA CHINA KUSHIRIKIANA USAFIRI WA RELI

 

  • I
    Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi Prof. Godius Kahyrara amesema Serikali
    ya Jamhuri ya Tanzania kwa kushirikiana Serikali ya China inatarajia
    kuliboresha Shirika la Reli la Tanzania na Zambia (TARAZA) ili kuliwezesha
    kuongeza ufanisi hususani katika usafirishaji wa mizigo.
    Prof. Kahyrara ameyasema hayo jijini Dodoma wakati aaliposaini mkataba wa
    Utendaji kazi na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) na
    kusisitiza kuwa tija ya maboresho hayo ni pamoja na kukuza pato pato la taifa
    na urahisi kwenye usafirishaji wa mzigo kutoka eneo moja kwenda jingine.
    “Shirika la TAZARA ni moja ya mashirika ambayo yanapewa kipaumbele kwa
    sasa hasa katika uboreshaji wa miundombinu ambayo kwa muda mrefu
    haikukarabatiwa na wenzetu wa Serikali ya China wameonyesha nia ya kusaidia
    kwenye eneo hilo” amesema Prof. Kahyrara.
    Katibu Mkuu Prof. Kahyrara amesema tayari Serikali imefanya maboresho
    katika Sheria ya Reli ili kuruhusu sekta binafsi kutoa huduma katika Reli ya
    TAZARA na TRC.
    Kwa upande wake Mkurugenzi wa TRC Bw. Masanja Kadogosa amesema
    miradi mbalimbali inaendelea kutekelezwa kwa reli ya Kati na Reli ya Kisasa
    ambayo hivi karibuni majaribio yatafanywa na kuanza kutoa huduma.
    Mkurugenzi Kadogosa ameongeza kuwa vitendea kazi kwa ajili ya uendeshaji
    wa SGR vimeendelea kuwasilia ambapo hivi karibuni TRC imepokea Kichwa
    kimoja cha reli hiyo kutoka Korea kusini ambapo kichwa hicho ni miongoni
    mwa Vichwa kumi na Saba ambavyo vimeagizwa.
    Naye Mkurugenzi wa Tathimini na Ufutiliaji kutoka Wizara ya Uchukuzi Bi.
    Devota Gabriel amemuhakikishia Katibu Mkuu Prof. Kahyarara kuwa kitengo
    hicho kimewekea mikakati thabiti itakayowezesha wataalam wa Wizara
    kusimamia kwa karibu miradi iliyopangwa kutekelezwa kwa mwaka wa fedha
    2023/2024 ili kuzingatia thamani na ubora.
    (Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Uchukuzi)


No comments