WAZIRI MKUU AZINDUA MASHINE YA KUCHANGANYA VIRUTUBISHO
Kassim Majaliwa amezindua mashine ya kuchanganya virutubisho kwenye vyakula na kuwaomba wadau wote wa maendeleo kuunga mkono juhudi hizo ili kuwezesha mashine hizo kuzalishwa kwa wingi kutumika katika maeneo yote hapa nchini.
Mashine iliyozinduliwa inatumika kuongeza virutubisho muhimu katika vyakula hususan unga wa mahindi, virutubisho hivyo ni pamoja na vitamin B na folic acid ambayo zinasaidia kwenye ukuaji wa watoto na kuzia kuzaliwa na changamoto za ulemavu ikiwemo mgongo wazi na vichwa vikubwa.

Post a Comment