WEZI WAMUIBIA KILEMA MALI ZA MILIONI 100
Kijana Aidan
Beltran ambaye ni mlemavu wa mwili, mwenye umri wa miaka 15, ameibiwa vifaa vyake
vyenye thamani ya dola za Marekani 50,000 sawa na fedha za Kitanzania zaidi ya
shilingi milioni 100.
Mama yake,
Alicia Rodriguez alisema kijana wake huyo aliibiwa baiskeli iliyotengenezwa
maalum kwa ajili yake na kiti chake cha kukalia kwenye gari, ambavyo vyote vina
thamani hiyo.
Tukio hilo
lilitokea huko Illinois nchini Marekani ambapo kiti hicho maalum kina thamani
ya dola 30,000 karibu shilingi milioni 70 na kiti cha gari kikiwa na thamani ya
dola 19,000 sawa na shilingi milioni 40.
Alicia ambaye
hana mume, amesema vifaa hivyo vilikuwa ni muhimu kwa mwanae ili aweze kuwahi
miadi ya madaktari wake ambao wamekuwa wakimtibu kwa muda wote kutokana na
kupooza.

Post a Comment