MSCL YAAGIZWA KUTAFUTA MASOKO
Kamati ya
kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) imemtaka
Mwenyekiti
wa bodi ya Kampuni ya Huduma za Meli (MSCL) kuhakikisha kitengo
cha masoko kinaanza
kutafuta
kampuni za kusafirisha
mzigo
kwenye meli
zinazojengwa
na kufanyiwa ukarabati ili kuziwezesha meli hizo kuanza kazi mara
moja baada
ya ujenzi na ukarabati kukamilika.
Akizungumza
mkoani Kigoma mara baada ya kukagua mradi wa ukarabati wa meli ya
MT. Sangara na eneo ambalo litajengwa chelezo kipya Mhe. Jerry Silaa amesema
uwekezaji
wa fedha uliowekwa hususani kwenye miradi ya ujenzi na ukarabati wa
meli unawapa
jukumu
kampuni
hiyo
kuhakikisha
wanapata
mzigo
wa
uhakika
utakaowawezesha
kupata fedha na hatimaye kuanza kujilipa mishahara na kuendesha
kampuni
bila kutegemea fedha kutoka Serikalini.
“Serikali
imeshaweka fedha nyingi kwenye kampuni hii, na kamati yetu ina jukumu la
kuhakikisha
mnapata
fedha
za
kuweza
kujiendesha
wenyewe
pasipo
kutegemea
ruzuku
kutoka Serikalini, mtafanikiwa kupata fedha mtaanza huduma za kusafirisha
mizigo
kupitia meli hizi’ amesema Mhe. Silaa.
Mhe. Silaa
ameitaka bodi hiyo kumlipa Mkandarasi Kampuni ya KTMI ambayo ndio
yenye kandarasi
ya
kujenga
meli
hiyo
ili
kuepuka
madeni
ambayo
yanaweza
kuzalishwa
kutokana na kucheleweshwa kwa malipo.
Aidha,
Mwenyekiti Mhe. Silaa ameipongeza Bodi, Menejimenti na Watumishi
wa
Kampuni hiyo kwa kusimamia
vyema miradi
inayotekelezwa na kuhakikisha
wahandisi
wake wanapata ujuzi ili kuweza kusimamia vyema meli hizo mara baada ya
ujenzi na
ukarabati kukamilika.
Kwa Upande
wake Mwenyekiti wa Bodi ya MSCL, Meja Jenerali Mst. John Mbungo
amemuhakikishia
Mwenyekiti
wa
Kamati
ya
PIC,
Mhe
Silaa
kuwa
mradi
huo
utakamilika
kwa wakati na tayari Kampuni imeshaweka mpango wa muda mfupi na
mrefu kwa
wa namna fedha iliyowekezwa inaweza kurudi kwa kuhakikisha mzigo wa
uhakika
unapatikana.
Naye
Mtendaji Mkuu wa MSCL, Eric Hamis amesema mradi wa ukarabati wa MT.
Sangara unatekelezwa
na
Kampuni
ya
KTMI
kutoka
nchini
Korea
Kusini
kwa
gharama ya takribani
shilingi
bilioni
8
na
kwa
sasa
umefikia
asilimia
90
na
unatarajiwa
kukamilika mapema mwezi April mwaka huu.
Eric
ameongeza kuwa miongoni mwa matokeo ya ukarabati huo mkubwa ni pamoja
kupungua
kwa masaa ya safari ambapo utaiwezesha meli hiyo kusafirisha mzigo kwa
saa 6 tu
ukilinganisha na hapo kabla ambapo ilikuwa inatumia saa zaidi ya 15 kwa
safari moja.
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa MItaji iko Mkoani Kigoma ambapo
imepokea taarifa
za
utendaji
wa
taasisi
za
WIzara
ya
Ujenzi
na
Uchukuzi
na
kutembelea
miradi inayotekelezwa kwa mwaka 2022/23.
(Imetolewa
na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi)






Post a Comment