URUSI WAMUAGA XI JINPING KWA AKUSHAMBULIA MIJI MITATU UKRAINE

 

Wakati Rais Xi Jinping wa China akiwa amemaliza mazungumzo na mwenzake Vladimir Putin, vikosi Vikosi vya Urusi vimeshambulia miji kadhaa ya Ukraine, na kuua watu wasiopungua watatu katika shambulio la ndege isiyo na rubani kwenye eneo la makazi la mkoa wa Kyiv.

Ghorofa za juu za majengo mawili ya makazi zilishambuliwa mapema Jumatano katika jiji la Rzhyshchiv, nje kidogo ya mji mkuu.

Mtoto wa miaka 11 alikuwa miongoni mwa waathiriwa kulingana na watoa huduma za uokoaji .

Kwengineko, maafisa wa jimbo la Crimea linalodhibitiwa na Urusi walisema shambulio la ndege isiyo na rubani ya Ukraine dhidi ya meli zao lilidhibitiwa.

Milipuko iliripotiwa na wakazi katika mji wa bandari wa Sevastopol.

Mkuu wa mamlaka ya uvamizi ya Urusi Mikhail Razvozhaev alisema "vitu" vitatu vilivyolenga Meli ya Bahari Nyeusi vimeharibiwa na meli za kivita za Urusi hazikuharibiwa.

Hakukuwa na maoni yoyote kutoka kwa jeshi la Ukraine, ambalo lilisema mapema wiki hii lilikuwa limeharibu makombora yaliyokuwa yanatumwa kwa meli hiyo katika kituo cha reli huko Dzhankoi kaskazini mwa Crimea.

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky alisema Urusi imerusha zaidi ya ndege 20 zisizo na rubani, pamoja na makombora.

Akizungumzia kuondoka kwa Rais wa China Xi Jinping kutoka Urusi saa kadhaa kabla, alisema kwamba kila wakati "mtu anapojaribu kusikia neno 'amani' huko Moscow," amri nyingine ilitolewa kuanzisha mashambulizi.

 


No comments