UGONJWA ULIOIBUKA KAGERA WATAMBULIKA


Serikali ya Tanzania imethibitisha kupatikana kwa virusi vya homa ya Marburg katika mkoa wa Kagera uliopo Kaskazini Magharibi mwa nchi hiyo.

Mnamo tarehe 16 March 2023, wizara ya afya ilitoa taarifa kwa umma juu ya ugonjwa ambao haukufahamika mara moja ambao uliambukizwa kwa watu mbalimbali.

Hata hivyo Tanzania imesema imefanikiwa kuuzuia ugonjwa huo kutoka nje ya mipaka ya mkoa wa Kagera.

Ugonjwa wa ajabu uliosababisha vifo vya watu watano kati ya wanane waliougua wilayani Bukoba Vijijini mkoani Kagera umetambuliwa kuwa ni Marburg.

Taarifa imesema ugonjwa huo huambukizwa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine au kutoka kwa mnyama kwenda kwa binadamu.



 

No comments