MBAPPE NAHODHA MPYA UFARANSA
Mshambuliaji wa Paris St-Germain Kylian Mbappe ameteuliwa kuwa
nahodha mpya wa Timu ya Taifa ya Ufaransa. Mbappe anarithi mikoba ya mlinda
mlango wa Tottenham, Hugo Lloris, ambaye alistaafu soka la kimataifa Januari
mwaka huu.
Mbappe, 24,
ameichezea Ufaransa michezo 66 tangu alipocheza mechi yake ya kwanza mwaka
2017.
"Kylian
anakidhi vigezo vyote vya kuwa na jukumu hili," kocha wa timu ya Ufaransa
Didier Deschamps alikiambia kituo cha televisheni cha Ufaransa TF1 katika
mahojiano yatakayorushwa Jumapili.
Shirikisho la Soka
la Ufaransa (FFF) lilithibitisha kuwa Deschamps amemteua Mbappe kama nahodha na
mshambuliaji wa Atletico Madrid, Antoine Griezmann kama nahodha msaidizi.
Mbappe alikuwa
mfungaji bora wa michuano ya Kombe la Dunia mwaka jana alipoisaidia Ufaransa
kufika fainali ya pili mfululizo ya Kombe la Dunia, ambapo walifungwa na
Argentina.
Alifunga mabao
mawili kwenye fainali ya 2018 dhidi ya Croatia na alitajwa kuwa mchezaji bora
chipukizi wa michuano hiyo huku Ufaransa wakitawazwa mabingwa wa dunia kwa mara
ya pili.


Post a Comment