TALIBAN WAOMBA KUTAMBULIWA KIMATAIFA, WAUA HARUSINI

 Afghanistan Taliban Conflict Which Islamic Countries In Favour Of Whom |  Afghanistan-Taliban Conflict: Know Which Islamic Country Is On Which Side?  Know Here

WAKATI wanamgambo wanaotawala Afghanistan wa Taliban wakiomba Jumuia za kimataifa kuwatambua na kuwapa misaada, watu watatu waliobeba silaha ambao wamejitambulisha kuwa ni Wanamgambo wa Taliban wamevamia harusini na kuamuru Muziki usimame kisha kuwaua Watu watatu na kuwajeruhi wengine kadhaa huku wakisema sababu ya kufanya hivyo ni kuzuia shughuli za Muziki ambazo zimepigwa marufuku nchini Afighanistan.

Msemaji wa Taliban Zabihullah Mujahid amesema Serikali haijahusika na mauaji hayo na kusema washambuliaji wawili kati ya watatu wamekamatwa na wanashikiliwa "Mtu akifanya mauaji hata kama ni Askari wetu tunamuona Mhalifu na tutamfikisha Mahakamani ili aadhibiwe"

Wanamgambo wa Taliban walitangaza kuzuia shughuli zote za Muziki baada ya kuchukua madaraka nchini Afighanistan wakisema ni kinyume na maadili ya Kiislamu.

No comments