SIMBACHAWENE AWATAKA WAMILIKI SILAHA KINYUME CHA SHERIA KUZISALIMISHA KWA HIARI

 Simbachawene replaces Lugola as Ilala's Zungu request granted - The Citizen

WAZIRI wa Mambo ya Ndani George Simbachawene ametoa siku 30 kuanzia November 01,2021 hadi November 30,2021 kwa Watu wanaomiliki silaha kinyume na sheria kuzisalimisha silaha zao na amesititiza kuwa watakaotii agizo hawatochukuliwa hatua.

"Natoa msamaha na usalimishaji wa silaha kwa wanaomiliki kinyume na sheria na ninawataka kuzisalimisha silaha hizo katika Vituo vyote vya Polisi, Ofisi za Serikali za Mitaa na kwa Watendaji wa Kata kuanzia saa 2 asubuhi hadi saa 10 jioni, Wahusika hawatoshtakiwa endapo watazisalimisha silaha hizo haramu kwa hiari na kwa muda uliopangwa"——— Simbachawene

"Baada ya muda uliowekwa kupita msako mkali utafanyika kwa Nchi nzima ili kuwakamata wote waliokaidi nafasi ya msamaha waliyopewa, zoezi hili litakuwa ni Mwezi November tu na atakayeshindwa kuwasilisha silaha ndani ya muda uliotamkwa atachukuliwa kama Mtuhumiwa"——— Simbachawene

No comments