SIMBA KUACHANA NA MAKOCHA WA KIZUNGU

 Inaweza kuwa picha ya Mtu 1 na maandishi yanayosema '1XBET ine.com 1XBET TOTAL 1XBE TOTAL 1X'

 

CEO wa Klabu ya Simba,Barbara Gonzalez amesema malengo ya Klabu ya Simba kwa Sasa ni kumwajiri Kocha wa Ki-Afrika na sio mzungu ili kuziba nafasi ya Didier Gomes ambaye waliachana naye hivi karibuni.

Inaelezwa kuwa Simba ipo kwenye mipango ya kumchukua Kocha Msaidizi wa Mamelodi Sundowns,Rulani Mokwena kuwa Kocha Mkuu wao.

"Suala la kocha halihitaji kukurupuka, kwani tunaweza kumpata mwenye wasifu mkubwa lakini akashindwa kutibu matatizo yaliyopo katika kikosi cha Simba na shida ikabaki pale pale,”

“Kama atakuwa Mokwena au mwingine hilo litajulikana ndani ya muda mfupi, lakini malengo ya klabu ni kumpata kocha kutoka Afrika na si Mzungu kama iliyetoka"

“Tunaweza kumpata kocha wa Afrika ambaye tunamuhitaji na wasifu wake usiwe mkubwa na akaweza kuisaidia timu kufikia malengo yake kwani atakuwa na kiu ya mafanikio na tutadumu naye kwa muda mrefu"

“Angalia klabu kama Chelsea wakati wanamchukua Thomas Tuchel wengi hawakuwa na imani naye, ila baada ya muda mfupi ameifanya timu kucheza vizuri na kushinda ubingwa wa Ulaya.”

 

No comments