RAIS WA ZANZIBAR AWAPA MASHAMBA WAKULIMA WETE

 Rais wa Zanzibar Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi amewasili Kisiwani Pemba kwa  ziara ya siku mbili | Presidents Office Zanzibar

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dr. Hussein Ali Mwinyi ametoa idhini ya mashamba ya karafuu maarufu kama mashamba ya EKA kupewa Wakulima na Wamiliki wanaoyahudumia badala ya mfumo wa sasa wa Serikali kuwakodishia.

Akizungumza na Wananchi kwenye ziara yake inayoendelea Kisiwani Pemba Dr. Mwinyi amesema Serikali imefikia uamuzi huo baada ya kuona hakuna haja ya kuendelea na mfumo wa zamani wa kuwakodishia mashamba Wakulima ili hali Serikali haiyahudumii.

Kuhusu ujenzi wa barabara ya Wete-Konde Mkoa wa Kaskazini Pemba, Rais Mwinyi amesema Serikali imeshatoa shilingi milioni mia saba (700) kwa ajili ya kuwalipa fidia Wakazi walioondolewa kupisha ujenzi wa barabara hiyo.

Jana September 1 2021 Rais Mwinyi amekua Rais wa pili wa Zanzibar baada ya Hayati Abeid Aman Karume kutembelea Kijiji cha Mleteeni kilichopo Wete Jimbo la Mtambwe Kaskazini Pemba ambacho hakijawahi kutembelewa na Kiongozi yeyote wa juu tangu mwaka 1969.

Rais  anaendelea na ziara yake leo Kisiwani Pemba kwa kukagua miradi ya maendeleo na kuzungumza na Wananchi katika Mkoa wa Kusini Pemba ambapo atatembelea Wilaya ya Chakechake.

 

No comments