RAIS SAMIA SULUHU HASSAN AKIRI WAHISANI KUSITISHA MISAADA

 Habarileo

RAIS Samia Suluhu Hassan amewaambia watanzania kwa sasa wahisani hawaleti misaada nchini, badala yake wanataka biashara ili kugawana faida

Amesema kwa sababu hiyo ni lazima tujinyang'anye wenyewe ili kufadhili miradi yetu.

Amesema hayo alipokuwa Tegeta akisalimia wananchi akiwa katika safari ya kuelekea Bagamoyo kutengeneza filamu ya kuitangaza Tanzania

Aidha Rais Samia Suluhu Hassan amesema mikopo ina riba kubwa na misaada imepungua, hivyo ni lazima wananchi kujichanga ili kujenga nchi

Amesema ni heri kuchukua mikopo kidogo kufadhili miradi mikubwa kama ya reli na umeme. Amesema hayo alipokuwa Zinga mkoani Pwani akielekea Bagamoyo.

No comments