RAIS SAMIA ASEMA TOZO NI KWA MAENDELEO, ZITAENDELEA KUWEPO

 Mzee wa Mshitu: MAKAMU WA RAIS SAMIA SULUHU HASSAN AMJULIA HALI MKUU WA  MAJESHI MSTAAFU JENERALI DAVID MSUGURI

 



SIKU chache baada ya tozo za miamala ya fedha katika mitandao ya simu kushuka kwa asilimia 30, Rais Samia Suluhu Hassan amesema Tozo zitaendelea kuwepo na hataki kuficha hilo.

Akizungumza na wananchi wa Tegeta, jimbo la Kawe jijini Dar es Salaam, amesema, "Tuliweka tozo kwenye mambo ya fedha za mitandao, yamepigiwa kelele sana, nimesikia. Nimekaa na wataalamu tumepunguza 30%. Miezi miwili tuliyoanza nayo tumekusanya kama Bilioni 60 na zimepelekwa kujenga Vituo 220 vya Afya"

"Januari tuna wimbi kubwa la Watoto wanataka kuingia Sekondari, lakini pia kuna wapya wanaoingia Darasa la Kwanza. Hakuna wa kutujengea ni sisi wenyewe. Fedha zitakazokusanywa Septemba na Oktoba zitaenda kujenga madarasa zaidi ya 500"

Katika hatua nyingine, Rais Samia amemuita kwenye gari Mbunge wa Kawe aliyeadhibiwa na Bunge, Askofu Josephat Gwajima, jambo lililomfanya ashangiliwe sana na wananchi.

Akiwa juu ya gari la Rais, Askofu Gwajima amesema wananchi wa Kawe siyo tu wanampenda mama Samia bali wana mahaba naye.

Wakati hayo yakiendelea, helkopta za Polisi zinaonekana juu ya anga katika kuhakikisha usalama.

Rais Samia amewataka wananchi waendelee kulipa kodi kwani kodi ni kwa maendeleo ya taifa.

Rais Samia amesema anaelekea Bagamoyo katika mtiririko wa uchukuaji picha ya filamu ya vivutio vya utalii wa Tanzania itakayozinduliwa nchini Marekani na kuonyeshwa dunia nzima.


No comments