POLISI WALALAMIKIWA KUNYANYASA WANAWAKE KINGONO HANDENI

 millardayo Twitterissä: "DC Gairo Siriel Mchembe ametoa Saa 24 kwa Kaimu  Mganga Mkuu Dr. Reuben Mfugale kuhakikisha ametenga vyumba maalum kwa ajili  ya kuhudumia Wagonjwa watakaopatikana na Virusi vya COVID19.  #MillardAyoUPDATES… https://t.co/WAvfT9ItTg"

WAKATI bado kukiwa na hisia tofauti juu ya ufanisi wa maadili na utendaji kazi kwa weledi wa baadhi ya askari Polisi, wanawake wilayani Handeni wamelalamika kuwa wananyanyaswa kingono na vijana hao wa IGP Simon Siro.
Mbele ya Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wa Wilaya, Sirieli Mchembe, wananchi hao wamesema unyanyasi wa baadhi ya Polisi hauvumiliki.
Mwanamke mmoja alisema..,. "Kuna Askari wakija humu ndani 'night club' wanatushika bila ridhaa yetu.. wanataka wanawake kilazima, akiona mwanamke anamkataa anamtafutia sababu anamkamata kwenda kumlaza selo"
Naye kijana wa kiume akamwagika... "Wakija humu ndani wanatufanyia jinsi wanavyotaka wao, demu wako mzuri anachukuliwa ukizingua unapigwa"
Mwananchi mwigine aliyesimama alisema "Anakuja na bunduki anaingia ndani mpaka Club humo ndani anachukua Mtoto wa kike anafanya vile anavyotaka, hata mimi siku hiyo nilikua natoka safari roho iliniuma na ukiangalia gari ya Polisi imepaki pale, anafanya unyama"
Baada ya Malalamiko hayo ya Wananchi Mkuu wa Wilaya Sirieli Mchembe alitoa tamko la Serikali huku akielezea tukio la hivi karibuni la mabinti wawili kupigwa na askari hao ndani ya moja ya kumbi za starehe zilizopo Wilayani Handeni jambo lililopelekea kuitisha mkutano nje ya ukumbi huo huku kura za siri zikipigwa kuwataja askari hao.
"Hakuna askari mwenye mamlaka ya kumgusa au kumchezea mwanamke maeneo yake bila kibali chake, cheo cha mtu hakihusiani na mwili wa mtu, mabinti wale watakuja hapa mtaona mmoja mpaka sasa hivi jicho limevimba wamepigwa mangumi ya hatari, Mimi kama DC Mwanamke unyanyasaji wa kijinsia Handeni hapana."

 

No comments