WANAJESHI 13 WA MAREKANI WALIPULIWA AFGHANISTAN

WANAJESHI 13 wa Marekani
wameripotiwa kupoteza maisha katiuka shambulio la bomu lililofanyika katika mji
mkuu wa Kabul, huko Afghanistan karibu na uwanja wa ndege.
Rais Joe Biden amesema Marekani
itaendelea kuwaondoa watu Kabul licha ya shambulio lililosababisha vifo vya wanajeshi
hao. Kwa mujibu wa Kituo cha Al Jazeera, raia wapatao 72 wamepoteza maisha.
Ameahidi kulipiza kisasi kufuatia kitendo hicho hawatosahau
wala kusamehe na wahusika watasakwa. Licha ya kutolewa tahadhari ya kutokea
shambulio, idadi kubwa ya watu walikusanyika eneo la Uwanja wa Ndege wa Kabul
wakitumaini kuruhusiwa kupanda Ndege.
Hadi sasa zaidi ya watu 100,000 wameshaondolewa Kabul
wakiwemo 66,000 kutoka Marekani.

Post a Comment