BEKI WA MAN CITY AFIKISHWA KORTINI KWA UBAKAJI

BEKI nyota wa Manchester City, Benjamin Mendy, 27, amefikishwa mahakamani leo akiwa amepakizwa katika karandinga ya polisi kujibu tuhuba za ubakaji na udhalilishaji wanawake.
Mlinzi huyo aliyejiunga kwa ada ya uhamisho wa paundi milioni 52 miaka minne iliyopita, anadaiwa kuwabaka wanawake watatu katika kipindi cha miezi kumi iliyopita, ndani ya jumba lake la kifahari lenye thamani ya paundi milioni 5.

Mchezaji huyo raia
wa Ufaransa anayelipwa paundi 90,000 kwa wiki, amesimamishwa na klabu yake kwa
sasa.
Mwanasoka huyo
aliwasili kortini Chester akiwa katika gari la magereza asubuhi ya leo.
Chanzo: Daily Mail

Post a Comment