MBUNGE SLAA AIKACHA KAMATI, YAOMBA IMKAMATE

MWENYEKITI wa Kamati ya Bunge ya Haki Maadili na Madaraka ya Bunge, Emmanuel Mwakasaka amesema ameomba kibali kwa Spika wa Bunge, Job Ndugai cha kukamatwa kwa mbunge wa Ukonga (CCM), Jerry Silaa baada ya kutofika katika shauri lake.
Silaa alihojiwa mara ya kwanza na kamati hiyo Agosti 24, 2021
ambapo mwenyekiti wa kamati hiyo Mwakasaka alimtaka kurudi tena leo Alhamisi
kuendelea na mahojiano.
Akizungumza na waandishi wa habari leo Alhamisi Agosti 26,
2021 mwenyekiti huyo alisema ameomba kibali cha kukamatwa kwa mbunge huyo baada
ya kutofika katika shauli lake.
Mwakasaka amesema Silaa hakutoa taarifa za kutofika kwake na
kwamba kamati hiyo ilimsubuiri hadi saa 8.00 mchana, hivyo wamemwomba Spika
kutoa kibali cha kukamatwa kwake na kufikishwa katika kikao cha kamati hiyo
kesho saa 4.00 asubuhi.

Post a Comment