BINTI AVAA KAMA BARMAID NA KUMUIBUKIA MAMAKE GROCERY BAADA YA COVID KUWATENGANISHA KWA MIEZI 18

BINTI mmoja nchini Uingereza amempa suprise mama yake baada ya kuvaa mavazi ya wahudumu wa baa na kumuibukia huku akiwa na kinywaji katika pub moja, miezi 18 baada ya kutoonana kutokana na vikwazo vya usafiri kutokana na janga la Covid 19.
Emma Nugent, wa Leeds,
hakuwa amemuona bintiye Sophie, kwa miezi 18 kwani kwa kuishi kwake Qatar
Sophie Nugent hakuwa na uwezo wa kumtembelea mama yake.
Mama alipatwa na
mshtuko baada ya kumuona bintiye akiwa katika mavazi ya wahudumu akimletea
kinywaji pale alipokuwa amekaa.
Mwalimu huyo
Mhispaniola anayeishi Doha, Qatar, Sophie Nugent, na mumewe, hakuwa na uwezo wa
kurejea England kutokana na vikwazo kwa zaidi ya mwaka kabla ya kuamua kurejea.
Alikata tiketi bila
kuwataarifu ndugu zake na kumshangaza mama yake akiwa na baba yake wa kambo,
Paul wakiwa wanapata kinywaji huko Rawdon, West Yorkshire.
Dada yake, Sasha alipiga video tukio hilo wakati mdogo wake akiwa amevaa shati jeupe na suruali nyeusi pomoja na miwani kama walivyokuwa wamevaa wahudumu wengine na akawafuata akiwa amevaa kinyago usoni ili kuficha utambulisho wake.


Post a Comment