BAADA YA KUMKOSA KANE, MAN CITRY WAMTAKA RONALDO

 

MABINGWA wa soka wa England, Manchester City, wamempa ofa mshambuliaji wa Juventus, Cristiano Ronaldo ya mkataba wa miaka miwili wa malipo ya pauni 230,000 kwa wiki, lakini wamekataa kuilipa timu yake ada ya uhamisho, baada ya Pep Guadiola kushindwa kumpata strika wa Spurs, Harry Kane

Mfungaji huyo wa Spurs aliuthibitisha Jumatano hii kuwa atabakia katika klabu yake.

Kikosi hicho cha Pep Guardiola kilimfukuzia mshambuliaji huyo wa Tottenham na nahodha wa England kwa msimu mzima, lakini fowadi huyo anayetajwa kuwa na thamani ya paundi milioni 150 alisema ana uhakika wa asilimia mia moja wa kubakia Spurs kwa msimu ujao.

Kwa kumkosa Kane, ina maana City ina watu wachache mbele baada ya kuondoka kwa Sergio Aguero. Gabriel Jesus ndiye mshambuliaji pekee wa kati ingawa wakati mwingine hucheza pembeni huku Ferran Torres na Liam Delap wakiweza pia kutumika.

 


No comments