CRISTIANO RONALDO ATUMIA DAKIKA 40 KUAGA JUVE

Ronaldo akiwasili katika uwanja wa mazoezi wa Juventus leo asubuhi
NYOTA raia wa
Ureno, Cristiano Ronaldo ameripotiwa kutumia dakika 40 kufika ofisi ya Juventus
na baadaye kwenda katika uwanja wa mazoezi kuwaaga wachezaji wenzake.
Ronaldo
ameshamalizana na kocha wa mabingwa wa England, Man City, Pep Gardiola na sasa
atakwenda kuwatumia miamba hao ambao ni wapinzani wakubwa wa timu yake ya
zamani ya Manchester United.
Mshambuliaji huyo
mwenye umri wa miaka 36 sasa, alikwenda mazoezini kuwaaga wenzake leo Ijumaa
asubuhi.

Post a Comment