WANAZI WA SIMBA 'WAMPA' SALUTE DOGO WA LUHANGWA


Inaweza kuwa picha ya Mtu 1, anacheza spoti, amesimama na nyasi

 DOGO muokota mipira katika Uwanja wa Soka wa Majaliwa uliopo Luhangwa mkoani Lindi, amewashika wanazi wa klabu ya Simba kwa namna alivyoonekana kutaka mabingwa hao watetezi waibuke na ushindi katika mechi yao dhidi ya Namungo.

Dogo huyo aliyekuwa nyuma ya lango la Namungo, mara kwa mara alionekana akirudisha mipira haraka ilipotoka upande wake ili kuzuia ucheleweshwaji wa muda na wakati John Bocco alipofunga bao lake la pili, uzalendo ulimshinda kiasi cha kujikuta akishangilia kwa nguvu.

Na hata bao la tatu lililofungwa na Morisson, almanusura aingie uwanjani kushangilia.

No comments