INAKUAJE UNAMUUA MKEO/MUMEO?


3 Things To Enhance Your Relationship With The Law Of Attraction


 MUME alirejea nyumbani kwa ajili ya chakula cha mchana akitokea kibaruani kwake. Kama ambavyo inakuwa siku zote, aliwapita akina mama majirani wakiwa wenye mashasha na, wakimuitikia kwa furaha salamu yake na wachache kati yao akitaniana nao.

Akaifikia nyumba yake na kuingia sebuleni. Hakumkuta mkewe hapo sebuleni na kama ilivyo kawaida, akaanza kuita, Baby...Baby...Baby... akielekea chumbani kwake.

Akamkuta mkewe akiwa amejilaza kitandani, kama mtu mwenye uchovu mwingi. Akiamini alijipumzisha kutokana na kazi nyingi za nyumbani, kwa kutumia simu yake, akampiga picha, kisha akambusu na kumuomba akamuandalie chakula mezani.

Wakatoka wote kuelekea sebuleni ambako baada ya mume kula na kushiba, akamshukuru mkewe na kisha huyooo, akaelekea zake kazini ambako hakukuwa mbali na nyumbani. Masaa mawili baadaye, akatoa simu yake na kuamua kumtazama mkewe katika picha aliyompiga.

Alitaka auone uzuri wake akiwa hajajipamba. Alitaka auone ubaya wa mkewe akiwa hajavaa sura ya vipodozi, alitaka aione sura yake ikiwa orijino. Ghafla akashtuka, mapigo ya moyo wake yakaanza kupiga kwa nguvu. Akaizoom picha. No....hakutaka kuamini.

Akaizima simu na kuiwasha tena. Akairudisha picha ya mkewe, akaitazama tena. Yes, alichokiona mwanzo ndicho alichokiona sasa. Hasira zikampanda, akaanza kutetemeka.

Kwenye kabati ofisini kwake, akaifungua na kutoa bastola yake. Akaifutika kiunoni, akatoka nje na kuipungia bodaboda, ikaja na kumpeleka nyumbani. Aliingia ndani kwake akiwa amevurugwa. Akamkuta mkewe sebuleni, tabasamu tele usoni.

Akapitiliza chumbani kwake, akalifunua godoro, hakuona kitu. Akarejea sebuleni kwake, akatoa bastola yake na mkewe akiwa ameduwaa, alishuhudia risasi ikipasua kichwa chake. Akafa palepale...

Kwa nini alimuua? Katika ile picha aliyompiga aliporudi kwa chakula, baada ya kuitazama vizuri, aliona kuna mwanaume alikuwa amejificha uvunguni mwa kitanda, akionekana sura kwa mbali. Alipoitazama vizuri, alimtambua mwanaume huyo, ni mtu anayemfahamu na kumheshimu!

Mlio wa risasi mbili pale sebuleni, iliwashtua majirani. Kwa tahadhari, wakafika nje na kuanza kubisha hodi. Mume alijitokeza akiwa amenyoosha mikono yake juu, tayari kuikabili hukumu yoyote iliyo mbele yake. Kuona hivyo, majirani wakaingia ndani na kushuhudia mwili wa mke ukiwa umelala sebuleni, damu nyingi zikivuja kutoka kichwani.

Wakajiuliza, nini kimetokea? Mbona dakika saa chache zilizopita, watu hawa wawili walikuwa na furaha tele?

Kipo kitu cha kujifunza. Mambo ya ndani ya nyumba, ni siri kubwa ambayo wakati mwingine hata watoto wa kuwazaa wasijue. Watoto wanaweza kuona wazazi wanagombana, lakini wasijue chanzo.

Yule mwanaume aliyekuwa ndani na marehemu, ni kaka wa mumewe, aliyekuwa akiishi jirani nao. Walikuwa na tabia za kutembeleana mara kwa mara na majirani wote walifahamu hivyo. Ni vipi walianzisha uhusiano wa kimapenzi na shemeji yake, si jambo muhimu kwa sasa. Lakini ujumbe ni kwamba usije ukasema haiwezekani kwa jambo lolote.

Tabia kama hizi, za mume kutembea na mdogo au dada wa mkewe au mke kutembea na mdogo au kaka wa mumewe, ni za kawaida katika jamii zetu. Achilia mbali kutembea na mume au mke wa rafiki yake, jirani yake au hata mfanyakazi mwenzake.

Na katika hali ya kushangaza zaidi, wapo watu wanatembea na wakwe zao, yaani mume au mke wa mwanaye. Kuna ushetani wa kutisha, kwani baadhi hutembea na hata watoto wao wa kuwazaa!

Na bahati mbaya sana, kwenye mahusiano haya, majirani huwa wanajua. Ni rahisi kumkuta mtu anakuambia, 'unamuona huyo mama, anatembea na shemeji yake' au 'huyo jamaa hapo bwana noma sana, anamla mdogo wa mkewe'.

Wanajuaje mahusiano haya, pia siyo jambo la msingi kwa sasa. Ujumbe wangu ni kwamba kuna mambo mengi sana machafu, yasiyo ya kimaadili tunayafanya huku mitaani, ambayo tukisikia tunayaona ya ajabu, wakati yanafanyika kila siku.

Kinachofanya wakati mwingine mume au mke kumuua mwenzake, wala siyo sababu za wivu wa kimapenzi kama tunavyopenda kurahisisha, bali ni kwa nini atembee na huyu? Mtu ambaye alikuwa akimchukulia kama spesho sana.

Chukulia kwa mfano wewe mume, mkeo anatembea na mdogo wako uliyemleta mjini ili aendelee na masomo. Kwa vyovyote, dogo hawezi kumtongoza shemeji yake, isipokuwa shemeji mtu alitengeneza mazingira ya kumshawishi bwana mdogo.

Au wewe mke, mumeo anatembea na mama yako mzazi. Kwa namna yoyote, alikuwa na kila sababu ya kukataa uhusiano huo kama alishawishiwa, lakini kwa kukubali, maana yake ni kuwa ameidhalilisha familia yao.

Ni kweli, katika uhusiano wa kimapenzi, zipo sababu nyingi zinazoweza kuwafanya watu wakorofishane, lakini nyingi kati ya hizo, husababishwa na uhusiano wa kimapenzi na watu wengine, hasa walio karibu yao!

 

No comments