ZIJUE ZINACHOJIVUNIA KLABU KONGWE ZA SOKA BONGO
1.
Young Africans Sports Club 'WANANCHI'
Ilianzishwa
rasmi siku ya Ijumaa tarehe 11 February 1935.
Awali
ilijulikana kama Italiana , New Young kabla ya hiyo Februari 11 1935
kujiita Dar es Salaam Young Africans au Yanga kwa matamshi ya Kiswahili.
Walianza
kutumia jezi za bluu ambapo pia wakijulikana kama The Navigators, ikiundwa na
wajanja wazawa waliokuwa mabaharia enzi hizo, wenyeji wa mitaa ya Jangwani,
jijini Dar es Salaam.
Jezi
zao za sasa ambazo ni rasmi za Njano, Kijani na Nyeusi walianza kuzitumia mwaka
1948.
Ndani
ya uwanja, Yanga wana rekodi kadhaa ambazo ni pamoja na kufika robo fainali
Klabu bingwa Afrika zamani ikiitwa African Cup of Champions Clubs mwaka 1969 na
1970 . Pia mwaka 1998 waliishia hatua ya makundi.
Katika
Michuano ya Kagame Cup, ambalo linashirikisha timu bingwa kutoka nchi za Afrika
Mashariki na Kati, inayoratibiwa na Baraza la Michezo la eneo hilo, CECAFA,
Yanga imelitwaa mara tano.
Katika
Michuano ya Kombe la Washindi Barani Afrika enzi hizo, ambalo sasa linajulikana
kama Michuano ya Shirikisho, Yanga imefika hatua ya makundi mara mbili, 2016 na
2018 na mwaka 1995, walifika hatua ya robo fainali.
Katika
Michuano ya Ligi Kuu Tanzania, ndiyo timu iliyobeba mataji mengi zaidi, ikiwa
ndiyo chanzo cha kuitwa mabingwa wa kihistoria, wakiwa wameweka kabatini kwao
mataji 27, huku wapinzani wao wa jadi, Simba ikiwa na mataji 22 tu.
Katika
michuano ya Kombe la Tusker, imetwaa mataji mawili, mwaka 2007 na 2009.
Makao makuu ya Jengo lao limejengwa na kampuni ya Mecco na kuzinduliwa rasmi April 1, 1974. Ndiyo klabu ya kwanza Tanzania kuwa na makao makuu yake yakiwa sambamba na uwanja wao ulioitwa Kaunda ambao kwa sasa hautumiki baada ya kukumbukwa na mafuriko ya mara kwa mara ya Mto Msimbazi.
2.
Simba Sports Club 'WEKUNDU WA MSIMBAZI'
Mwaka
mmoja baada ya kuzaliwa Yanga SC nchini Tanzania (Tanganyika ), mwishoni mwa
mwaka 1935 kuliibuka ugomvi mkubwa ndani ya klabu hiyo ya Jangwani, hususani
katika mfumo wa uendeshaji na umiliki wake ambao ulisababisha baadhi ya watu
kujiondoa na kwenda kuanzisha klabu yao.
Ugomvi
huo ulichochewa sana na Serikali ya kikoloni enzi hizo katika kuvunja umoja wa
Watanganyika kupitia michezo. Wakiitekeleza vema ile dhana ya DIVIDE AND RULE
yaani wagawe ili uwatawale vizuri.
Hii
ilipelekea kuibuka kwa Queens SC ambao ndiyo hasa chimbuko la Simba SC, hiyo
ikiwa ni tarehe 17 March 1936, ambao ni muda wa kama mwaka mmoja na miezi
miwili baada ya kuanzishwa kwa Yanga.
Jina
hilo halikuwavutia wengi kutokana na mikogo kwa wapinzani wao, Dar es Salaam
Young Africans hivyo mwaka 1942 walibadilisha jina lao na kujiita The Eagles .
Walijiita
The Eagles mwaka huo wakiwa daraja la pili sambamba na Yanga SC na klabu
zingine.
Eagles
walikuwa vyema katika vifaa na jezi mbalimbali, wakitumia jezi nyeusi zenye
michirizi miyekundu huku jezi nyeupe ikiwa ni jezi yao mbadala.
Mwaka
1965 baada ya kuanzishwa rasmi ligi daraja la kwanza ambalo lilikuwa
likishirikisha timu za bara na visiwani baada ya Muungano wa mwaka 1964, Eagles
walibadili jina na kujiita Sunderland.
Mwaka
1968 hayati Abeid Amani Karume, rais wa kwanza wa Zanzibar, alionesha mapenzi
makubwa katika soka nchini, baada ya kutoa ufadhili kwa klabu za Bara na
Visiwani.
Ikumbukwe
kwa nyakati tofauti aliziwezesha African Sports ya Zanzibar, Mlandege, African Sports
ya Tanga na Yanga SC kujiinua kiuchumia, kama alivyofanya pia kwa
Sunderland.
Miaka
miwili baadaye, yaani mwaka 1970 alitoa wazo la klabu zenye majina ya kizungu
kubadili majina yao, akipendekeza Sunderland kuitwa Simba wa Afrika ). Ni
Agosti 8, 1972 ndipo Sunderland ikafa rasmi na kuanza kutumika kwa jina la
SIMBA SPORTS CLUB.
Katika
historia ya Ligi Kuu Tanzania Bara ambayo zamani ilijulikana kama ligi daraja
la kwanza, Simba ndiyo ilikua klabu ya kwanza kutwaa taji hilo, ikifanya hivyo
mwaka 1965. Lakini wameweza kuchukua kombe hilo mara 22 tu, nyuma ya Yanga SC
walioweza kufanya hivyo mara 27.
Ndiyo
vinara wa michuano ya Kagame Cup, inayoshirikisha timu kutoka nchi za Afrika
Mashariki na Kati, ikiwa imetwaa taji hilo mara sita, nyingi kuliko timu
nyingine yoyote.
Ndiyo
klabu pekee kutoka Tanzania kuwahi kucheza fainali za michuano ya Afrika,
ikifanya hivyo mwaka 1993, ilipokosa kombe mbele ya Stella Abdjan ya Ivory
Coast, ambalo sasa linaitwa Kombe la Shirikisho.
Katika
michuano ya kombe la Tusker, timu hiyo wamelichukua mara nne, miaka ya 2001,
2002 , 2003 na 2005.
Wana
rekodi ya kufika hatua ya robo fainali klabu bingwa Afrika mara tatu, mwaka
1994, 2018-19 na mwaka huu. Ina nafasi ya kuwa klabu ya kwanza Tanzania
kuandika rekodi ya kufika nusu fainali ya Klabu Bingwa Afrika endapo itaitoa
Kaizer Chiefs inayokutana nayo katika hatua ya robo fainali.
3.
African Sports Club 'WANA KIMANUMANU'
Hawa
ni watoto wa jijini Tanga walioanzisha timu yao Julai 12, 1936 miezi michache
baada ya kuanzishwa Simba SC jijini Dar es Salaam.
Africans
Sports ni matokeo ya mapinduzi ya kukua kwa mwamko wa soka Tanganyika
yaliyoanzia jijini Dar es Salaam baada ya kuzaliwa Yanga na Queens (Simba SC).
Wazee
wa Tanga waliamua nao kuanzisha timu yao ili kupata nafasi ya kushiriki
michuano ya ligi ya Pwani iliyotawaliwa sana na timu za Dar es Salaam.
Hawa
walikuwa na undugu na Yanga ya jijini Dar es Salaam pia African Sports ya
Zanzibar. Walitumia jezi zilizofanana.
Ndani
ya uwanja, hawa ni mabingwa wa Ligi Kuu ya Muungano mwaka 1988, wakiwa wameanza
kucheza ligi ya daraja la kwanza mwaka 1965 na kushuka mwaka 1991 kabla
ya kurejea tena mwaka 2015 baada ya kupita miaka 23 lakini kwa sasa imeshuka
tena daraja.
Historia
yao inaanzia mwaka 1932 barabara ya 12 jijini Tanga . Hapo ndipo walipoanza
kuisuka timu yao kabla ya mwaka 1936 kupata leseni ya kuwa klabu rasmi ya mpira
na michezo mingine.
4.
Coastal Union 'WAGOSI WA KAYA'
Wagosi
wa Kaya, walianzishwa rasmi mwaka 1948 wakitokea ubavuni mwa African Sports
kama ilivyo kwa Simba SC na Yanga SC .
Hawa
ni mabingwa wa Nyerere Cup mwaka 1980 na 1988.
Mabingwa
wa Ligi kuu Tanzania Bara mwaka 1988 wakashindwa kutetea kombe hilo mwaka 1989
ambapo lilikwenda kwa Malindi ya Zanzibar. (Wakati huo kukiwa na Ligi Kuu ya
Muungano)
Ni
wapinzani wa Jadi wa African Sports huku wakiwa na undugu wa miongo kadhaa na
Simba SC hali inayowafanya kuwa pia na upinzani na Yanga SC ambao wana undugu
na African Sports.
Mwaka
1981 walijitoa Ushiriki wao klabu bingwa Afrika lakini waliweza kushiriki mwaka
1989 na kuondolewa hatua za awali. Walijitoa mwaka 1981 kutokana na Ukata.
Credit
kwa Samuel Samuel wa Futbal Planet FB

Post a Comment