CRISTIANO RONALDO: MWANASOKA TAJIRI MWENYE MOYO WA KUTOA AKIGUSWA


Cristiano Ronaldo | Biography & Facts | Britannica

KUNA wanasoka wengi waliopata pesa kutokana na uwezo wao uwanjani, wakilipwa mamilioni kila siku, wiki, mwezi na kwa mwaka. Miongoni mwa hao, ni Mreno, Cristiano Ronaldo ambaye ni tajiri miongoni mwa wachezaji wakubwa duniani.

Amefanya mengi kuthibitisha namna anavyoguswa na matatizo ya watu wengine, hasa wale ambao hawana uwezo kama wake.


Miaka kadhaa nyuma uwanjani Estadio Di Dragao Jijini Lisbon Ureno, wakati timu ya taifa ya Ureno ikifanya mazoezi, ghafla aliingia mchezaji Carlos Martins ambaye alionekana mnyonge sana, Ronaldo alikuwa wa kwanza kumfuata.

Alimuuliza Martins shida nini? Martins alieleza kuwa mwanae anaumwa sana, ana upungufu wa bone marrows (uroto) anapaswa kuchangiwa, Ronaldo bila kusita akahimiza na wachezaji wengine wakaelekea hospital kumchangia kijana.

Mwaka 2007, Cristiano Ronaldo alilazimika kusafiri mpaka Asia, baada ya mwandishi mmoja kumpiga picha mtoto alietelekezwa wakati wa Tsunami kali, mtoto alikuwa na jezi ya Ronaldo mgongoni, hiyo ilimgusa sana na anamsomesha mpaka leo, yupo Ureno

Miaka kadhaa mbele, aliwahi kuhojiwa Cristiano Ronaldo kwanini hana mchoro wowote mwilini (tattoo) aliweka wazi kuwa adhma yake ni kuwa Mchangiaji wa damu kwa maisha yake yote, angechora tattoo maana yake angekosa sifa ya kuchangia.

Mwaka 2011 baada ya kubeba kiatu cha dhahabu cha wafungaji Bara la Ulaya, wakati anarudi nyumbani alisikia taarifa redioni juu ya uhaba wa huduma za Kijamii kule Ukanda wa Gaza, changamoto ya shule, hospital na maji.

Ronaldo alimuagiza wakala wake, Jorge Mendez achukue kiatu chake cha dhahabu kikapigwe mnada kisha pesa ile yote ipelekwe Gaza, ilipatikana kweli Pauni 1.5 Million na Mendez akaipeleka Gaza ili iwasaidie watoto kule kupata huduma zote za kijamii kwa wakati sahihi

Wakati shirika la SAVE THE CHILDREN linapambana kusaidia watoto nchini Nepal 2015, Ronaldo aliguswa mno na harakati zile, ikalazimika asaini cheki ya Pauni Million 5, pesa hiyo ilisaidia kwa asilimia kubwa kwa watoto kule nchini Nepal.
Juzi kile kitambaa alichotupa kwa hasira pale Serbia kiliokotwa na Mfanyakazi wa uwanja huo na kukipeleka kwenye Asasi za Kijamii na kikapigwa mnada kusaidia upasuaji wa watoto kule Belgrade, na inasemekana kiliuzwa kwa bei ya juu sana.

Credit: Shaffi Dauda

No comments