RIPOTI YA CAG INACHANGANYA

 

RIPOTI ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) inayoonyesha ufisadi wa kiwango cha juu cha fedha za serikali, umewachanganya wananchi, wasiamini kama jambo hilo limeweza kufanyika enzi za utawala wa Rais wa Awamu ya Tano, John Pombe Magufuli.

Katika ripoti hiyo, imeonyesha ufisadi katika baadhi ya maeneo ambayo inaaminika yalikuwa chini ya uangalizi makini wa JPM mwenyewe, kama ATCL ambako shilingi zaidi ya bilioni tatu 'zilipigwa' kwa ajili ya matengenezo ya ndege, ambayo kumbe imepaki tangu mwaka 2015.

Hiyo ni mbali na hasara ya zaidi ya shilingi bilioni 153 ndani ya miaka mitano ya utawala wa kiongozi huyo aliyekuwa na sifa ya ukali.

Aidha, serikali imepata hasara ya mabilioni katika mradi wa Bwawa la Umeme la Mto Rufiji, baada ya kubainika wageni zaidi ya 1500 wanafanya kazi bila kuwa na vibali vya kuwaruhusu kufanya kazi nchini.

Eneo jingine lililowachanganya wananchi, ni ripoti kuwa fedha zilizopigwa na wajanja, zilipitia katika akaunti ya Jeshi la Uokoaji, jambo ambalo haieleweki ni katika mazingira gani jambo hilo liliwezekana.

 

No comments