David Cameron afanya mazungumzo Israel kupinga vita na Iran
David Cameron ameitaka Israel kufanya "kila iwezekanavyo ili kupunguza" wasiwasi Mashariki ya Kati, kabla ya mazungumzo na Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu.
Israel imeapa kulipiza kisasi baada ya shambulio la Iran la kombora na ndege zisizo na rubani mwishoni mwa juma.
Waziri wa mambo ya nje wa Uingereza ataishinikiza Israel kudhibiti kiwango cha mwitikio wake kutokana na hofu kwamba inaweza kusababisha vita zaidi.
Alitoa wito kwa serikali ya Israel kuwa "mwerevu na vile vile imara".
Akizungumza na waandishi wa habari muda mfupi baada ya kuwasili Jerusalem siku ya Jumatano, Bwana Cameron alisema alikuwa huko "kuonyesha mshikamano baada ya shambulio hilo baya la Iran".
Aliendelea: "Ni sawa kuweka maoni yetu wazi juu ya nini kinapaswa kutokea baadaye, lakini ni wazi Waisraeli wanafanya uamuzi wa kuchukua hatua.
"Tunatumai watafanya hivyo kwa njia ambayo haitazidisha mzozo. Na kwa njia ambayo, kama nilivyosema jana, ni busara na thabiti.
"Lakini hitaji la kweli ni kuangazia tena Hamas, kurejelea suala la mateka, msaada wa kibinadamu, kurejelea mazungumzo ya kusitishwa kwa mzozo wa Gaza."
Baadaye, Bwana Cameron atasafiri kwenye mkutano wa mawaziri wa G7 nchini Italia, ambapo atashinikiza kuratibiwa kwa vikwazo dhidi ya Iran.
Ameishutumu Tehran kwa kuwa "nyuma ya shughuli nyingi mbaya" katika Mashariki ya Kati na kutoa wito kwa nchi nyingine kuchukua hatua zilizopangwa kuzuia ushawishi wa Iran.
BBC

Post a Comment