Yanga: Mzunguko bure mechi ya Mamelodi
Kuelekea
mechi ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Barani Afrika dhidi ya Mamelodi
Sundowns ya Afrika Kusini, miamba ya soka nchini, Yanga, imetangaza kuwa
mashabiki watakaokaa mzunguko wataingia bure.
Afisa
Habari wa Yanga, Ali Kamwe amesema katika maeneo mengine ndani ya Uwanja wa Benjamin
Mkapa, mashabiki watalipia. Watakaokaa VIP A watanunua tiketi kwa shilingi
30,000, wale wa VIP B watatoa 20,000 na katika VIP C watapata burudani ya buku
teni tu.
Kuhusu
hali ya kiungo wao tegemezi, Pacome Zouazoua ambaye alipata majeraha katika
mechi iliyopoteza dhidi ya Azam, hali yake bado haijakaa sawa, akifafanua kuwa
madaktari wa timu ya taifa ya Ivory Coast, ambao wamemuita kambini Ufaransa,
wamemuomba huko ili waone nini wanaweza kumsaidia.
Alisema
madaktari hao watawataarifu kuhusu hilo na wao kama klabu watatoa taarifa.
Aidha, mlinzi Yao Kouassi aliyepata majeraha pia katika mechi hiyo hali yake
bado ni hamsini kwa hamsini wakati Daktari wa Boli, Khalid Aucho yeye
anaendelea kuimarika na beki wao Kibwana Shomari anaripotiwa kuwa ataanza
mazoezi Jumatatu ijayo.

Post a Comment