CAG Kichere: Licha ya kupewa Ruzuku ya Tsh. Bilioni 31.55, ATCL imepata hasara ya Tsh. Bilioni 56.64, ongezeko la 61% kutoka hasara ya Mwaka 2021/22

 

Ukaguzi umebaini MSD ilitoa zabuni ya ununuzi wa vifaa vya maabara ambavyo ni vipimo vya COVID 19 kwa kampuni ambayo haikuwa mtengenezaji wa vifaa hivyo kinyume na makatwa ya zabuni, pia ilinunua vifaa hivyo bila kufuata ushauri, baada ya kufika kwa vifaa hivyo wataalamu walibaini havifai kwa matumizi yetu na tayari MSD ilikuwa imelipa fedha zote.

Mashirika ya Umma yanayojiendesha kibiashara yamepata hasara. Mwaka 2022/23, ATCL imepata hasara ya Tsh. Bilioni 56.64, sawa na ongezeko la 61% kutoka hasara ya Mwaka 2021/22 iliyokuwa Tsh. Bilioni 35.24. Ikumbukwe kuwa Shirika hili lilipokea ruzuku ya Tsh. Bilioni 31.55 kutoka Serikalini.

Shirika la reli limepata hasara ya Tsh. Bilioni 100.70 licha ya kupewa ruzuku ya Tsh. Bilioni 32.81 kutoka Serikalini.

TANOIL imepata hasara ya Tsh. Bilioni 76.56, ongezeko la Bilioni 68.72 kutoka hasara ya mwaka 2021/22.

Shirika la Posta limepata hasara ya Tsh. Bilioni 1.34.

NHIF umeendelea kupata hasa kwa mwaka wa 5 mfululizo ambapo mwaka 2022/23 umepata hasara ya Tsh. Bilioni 156.77. Hata hivyo, NHIF imeikopesha Serikali Bilioni 208 ambazo hazijalipwa hadi sasa.

No comments