Mike Iron Tyson, Evander wakutana baada ya miaka 27

 


Hatimaye Mike BondiaTyson na Evander Holyfield wameonesha kuwa hawana tofauti na wamedhihirisha kuwa sasa kuwa imani ipo kati yao baada ya kupozi kwenye picha ya pamoja, ikiwa ni miaka 27 tangu pambano lao lifanyike ambapo katika pambano hilo Bondia Tyson alimng’ata sikio Evander na kupelekea kupoteza pambano hilo mwaka 1997.
Kupitia chapisho rasmi ya instagram kwenye account ya Mike Tyson alichapisha picha hiyo na kuandika ["We've come a long way since the bite fight”] akiwa na maana ya["Tumetoka mbali sana tangu kupigana kwa kung’atana"]
Baada ya pambano hilo, imepita miaka mingi sasa kukiwa na hali ya kutokuelewana kati yao lakini picha hiyo ya pamoja imeonesha kufuta tofauti zao za muda mrefu.

Inakumbukwa kuwa Tyson ndiye aliyemng'ata sikio Holyfield kwa mshtuko lakini alitupwa nje na mwamuzi Mills Lane. Hata hivyo, Tyson alipomng’ata tena sikio mpinzani wake, mara moja alienguliwa na kusababisha tukio hilo baya ulingoni huku akiambulia kupoteza pambano hilo.
Credit: TBConline

No comments