BASHUNGWA AAGIZA WAHANDISI KUONGEZEWA WIGO
Waziri wa Ujenzi, Innocent
Bashungwa ameiagiza Bodi ya Usajili ya Wahandisi (ERB) kuongeza wigo wa
kuwajengea uwezo Wahandisi Washauri nchini ili kuhakikisha utalaam na ujuzi
unakuzwa kwa maendeleo ya nchi.
Bashungwa amezungumza hayo
jijini Dodoma katika mkutano uliokutanisha Mwenyekiti na Wajumbe wa Bodi ya
Usajili ya Wahandisi (ERB), na kusisitiza kuweka mikakati mahususi ya
uendelezaji wa Wahandisi Washauri kitaaluma ili kukuza tasnia ya Uhandisi.
“Vipaumbele na maagizo ya
Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
katika sekta hii ni kuona ushiriki mkubwa wa Wahandisi na Makandarasi Wazawa
katika kazi za ujenzi na usimamizi wa miradi (Local Content), sisi kama
wasaidizi wake tuhakikishe tunalitekeleza hili”, amesema Bashungwa.
Aidha, ameelekeza
kuhakikisha kunakuwa na uwepo wa ushirikishwaji wa Wahandisi wahitimu katika
mpango wa mafunzo kwa vitendo (SEAP) kwenye miradi mikubwa inayotekelezwa
nchini ili kuwajengea uwezo.
Vilevile, ameagiza kuangalia maeneo yote yenye changamoto katika Sheria ya Usajili ili kuwawezesha wahandisi kufanya ubunifu na kusaidia nchi katika uchumi wa viwanda na maendeleo ya Sayansi na Teknolojia

Post a Comment