Maneno azikwa nyumbani kwake Chalibze


Mazishi ya aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Pwani Marehemu Ramadhani Maneno  kwa kipindi Cha 2017  hadi 2022 yamehitimishwa  leo Alhamis Januari 4, 2024 saa saba na nusu mchana tarehe nyumbani kwake Chalinze.


Mazishi hayo yamehudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa Chama na Serikali akiwemo Mhe, Daktari Jakaya Mrisho Kikwete,  Raisi mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania awamu ya nne.


Aidha Mhe, Daktari Samia Suluhu Hassan, Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika msiba huo ametuma salamu za Rambirambi na kutoa ubani wa  Shilingi milioni 10.


 Taarifa hii imeandaliwa na


David Mramba

Katibu wa Siasa na Uenezi CCM

Mkoa wa Pwani.

No comments