Katibu Mkuu TAMISEMI atoa maagizo kwa maofisa elimu
Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Adolf Ndunguru amewaagiza Maafisa elimu wote wa Mikoa na Halmashauri hapa Nchini kukamilisha ujenzi wa miradi ya Elimu inayotekelezwa katika maeneo yao kabla au ifikapo Januari 15, mwaka huu.
Katibu Mkuu huyo ametoa maqgizo hayo Januari 4, 2024 wakati akifungua kikao kazi cha Makatibu Tawala wasaidizi Idara ya Elimu pamoja na Maafisa Elimu wa Halmashauri kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa hoteli ya Glonency iliyopo Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.
Kikao kazi hicho kilichokuwa na kauli mbiu isemayo, uwajibikaji wenye ubora ubunifu na uadilifu ni msingi muhimu katika kuboresha elimu msingi na sekondari Nchini kinalenga kuweka mikakati ya pamoja kwa ajili ya mwaka 2024, ili kuweza kusimamia masuala ya elimu na kupata mafanikio.
Aidha, Aldof Ndunguru amewataka Maafisa hao kusimamia kikamilifu ufundishaji na ujifunzaji mashuleni na kuhakikisha walimu wasiotimiza wajibu wao kuchukuliwa hatua stahiki, pia kuhakikisha wanafunzi wote wa darasa la tatu na kidato cha kwanza wanamudu stadi ya lugha ya kingereza ifikapo mwishoni mwa mwaka.
“….. Hakikisheni miradi yote inayotekelezwa kwenye maeneo yenu ya usimamizi inakamilika kabla au ifikapo januari, 15 2024...” amesema Adolf Ndunguru.
Pia Ndungulu amesema chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan tunashuhudia uwezeshaji mkubwa wa rasilimali fedha katika sekta ya Elimu hapa Nchini kwa kugharamia elimu msingi bila ada ya shilingi bilioni 33.3 kila mwezi na kupanua wigo wake hadi kufika kidato cha sita.

Post a Comment