Kashfa iliyomkumba TB Joshua inavyowatafuna manabii Tanzania

 

Na Mwandishi Wetu

Wakati dunia ikiwa bado haiamini kile kinachoendelea kuibuliwa na Shirika la Utangazaji la Uingereza BBC, juu ya udanganyifu na hila zilizokuwa zikitumiwa na TB Joshua, mmoja wa wahubiri aliyepata umaarufu mkubwa duniani, hali imekua tete kwa watumishi wa Mungu wanaofanya shughuli zao nchini Tanzania.


BBC imefichua, kwa mara ya kwanza, jinsi mwinjilisti wa televisheni wa Nigeria marehemu TB Joshua alivyoghushi miujiza iliyovutia mamilioni ya watu kwenye kanisa lake.

Mhubiri huyo, ambaye anatuhumiwa kwa unyanyasaji na utesaji ulioenea kwa takriban miaka 20 , alianzisha Kanisa lake la Synagogue Church of All Nations (SCOAN) mjini Lagos zaidi ya miongo mitatu iliyopita. Kuinuka kwake kwa umaarufu kulifungamanishwa kwa karibu na uwezo wake wa kujidai wa kuwa na nguvu za kimungu na uwezo wake unaodhaniwa kuwa wa kuponya wagonjwa.

Hapa Tanzania, wapo wahubiri ambao nao wamejipa uwezo huo na kuwafanya kuwa na mamia kwa maelfu ya wafuasi. Baadhi ya watumishi hao wa Mungu, kama alivyokuwa TB Joshua, wamekuwa wakifanya miujiza ya kuwainua watu waliolala kwa kushindwa kutembea, kuponya magonjwa yaliyoshindikana na hata kusaidia watu kupata vyeo makazini na mafanikio katika biashara zao.

Baadhi ya waumini hao waliozungumza na Ojuku Blog, wameelezea kushtushwa kwao na taarifa za udanganyifu wa TB Joshua, kwani hata mhubiri wao, alisema alipata nguvu za upako kutoka kwa mtumishi huyo raia wa Nigeria.

“Kwa kweli inabidi tujitafakari upya. Hiki kinachotokea Nigeria kinatupa tafakuri sana maana naona kama mambo yanafanana. Serikali itusaidie kuchunguza huenda na sisi tunaibiwa bila kujijua,” anasema muumini wa kanisa moja linaloshuhudia miujiza kila mwisho wa wiki katika kanisa wanalosali, ambalo kwa sasa linahigadhiwa.

Mwanaharakati mmoja ambaye hataki jina lake litajwe, anaiambia blog hii kuwa manabii wengi nchi hii ni wa uongo na kwamba wanafanikiwa zaidi kutokana na wananchi wengi kukata tamaa na hivyo kujikuta wakitaka kufanikiwa kwa njia za mkato.

“Wee hebu jiulize, anaonekana mwanamke ambaye hata kiswahili tu hawezi, anasema mtoto wake alijisaidia kwa njia ya haja kubwa eti sijui mjusi, nyembe na nini sijui. Sasa kule kijijini eti anapiga picha yupo kwenye choo cha sinki, lakini ukimtazama, huamini kama hata anajua kutumia smartphone. Ni utapeli tu umejaa,” anasema.

 

No comments