MRADI WA UBORESHAJI WA MTO MSIMBAZI UTATATUA CHANGAMOTO ZA MIAKA 100 IJAYO
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa amesema katika mradi wa Uboreshaji wa Mto Msimbaza unaotegemewa kuanza hivi karibu utatatua changamoto za miaka 100 ijayo na sio baada ya miaka 10 tena tunaanza kukutana na changamoto kama hizi.
Hayo yamesemwa leo tarehe 13.11.2023 wakati wa ziara ya pamoja ya Mawaziri wa Wizara tatu ambazo zimetembelea eneo la Jangwani ambalo limathirika na mvua zinazoendelea kunyesha baada ya Mto Msimbazi kujaa.
Wizara hizo ni Ofisi ya Rais- TAMISEMI, Wizara ya Ujenzi pamoja na Wizara ya Fedha.
Amesema tayari Serikali kupitia OR-TAMISEMI imesaini mkataba wa kupata fedha kutoka Benki ya Dunia zitakazo wezesha kutekeleza mradi mkubwa wa uboreshaji wa Bonde la Mto Msimbazi ikiwa ni pamoja na kujenga daraja la juu litakaloanzia eneo la Magomeni hadi njia panda ya Muhimbili (Fire) ambao umepangwa kuanza Februari 2024.

Post a Comment