ZITTO AWA WA KWANZA KUMLIPA MAMA, ACT HAITASIMAMISHA MGOMBEA 2025
Kiongozi Mkuu wa chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe amekuwa wa kwanza kulipa fadhila za maridhiano kati ya Serikali na vyama vya upinzani, baada ya kutangaza kuwa hatagombea katika Uchaguzi Mkuu ujao na badala yake atafanya hivyo mwaka 2030.
Katika andiko lililopatikana kwenye mtandao wake wa kijamii, Zitto alisema kwa heshima waliyopewa, wao kama ACT wameamua kumlipa kwa kutosimamisha mgombea wakati huo, akisema badala yake watawekeza nguvu kubwa katika kuwapata wabunge wengi, ili wawe chama kikuu cha upinzani bungeni, ambacho wabunge wake hawatasusia Bunge la Katiba.
Hata hivyo, Chadema hawajasema chochote kuhusiana na kusimamisha au kutosimamisha mgombea katika uchaguzi ujao.



Post a Comment