MZEE WA KIPALESTINA AONYESHA HATI YA UMILIKI WA PALESTINA KUTOKA KWA OTTOMAN
Picha ya mkulima wa Kipalestina huko Jurish akiwa ameshikilia
hati ya mauzo ya miaka 117 iliyo na muhuri wa Ottoman inayothibitisha kwamba
ardhi hiyo ni ya familia yake.
Mpalestina huyu mwenye umri wa miaka 73 alisema kwamba hati hii, iliyorithiwa
kutoka kwa babu yake, ilihifadhiwa kutoka kizazi hadi kizazi katika sura ya
plastiki yenye kingo zilizovunjika.
"Hii ni hati ya kipindi cha Uthmaniyya inayoonyesha kuwa babu yangu
'Abdulfettah Mansour alinunua ekari 60 za ardhi huko Jurish. Hati hiyo
inathibitisha kwamba ardhi ilinunuliwa na 'Abdulfettah Mansour.
Pia kuna muhuri wa Ottoman chini. Ardhi hii inamilikiwa na familia yetu tangu
1906." Picha ya mkulima wa Kipalestina huko Jurish akiwa ameshikilia hati
ya mauzo ya miaka 117 iliyo na mhuri wa Ottoman inayothibitisha kwamba ardhi
hiyo ni ya familia yake.
Ottoman, mtawala wa kibabe wa maeneo mengi
barani Ulaya, Asia na Afrika, aliitawala Mashariki ya Kati tangu karne ya 14,
ikijulikana ka Boma ya Ottoman (Ottoman Empire). Utawala wake ulianza kufifia
mwishoni mwa karne ya 17 na mwanzoni mwa 18, hasa baada ya kifo cha kiongozi
wake, Suleiman
the Magnificent


Post a Comment