MZEE WA KIPALESTINA AONYESHA HATI YA UMILIKI WA PALESTINA KUTOKA KWA OTTOMAN

Picha ya mkulima wa Kipalestina huko Jurish akiwa ameshikilia hati ya mauzo ya miaka 117 iliyo na muhuri wa Ottoman inayothibitisha kwamba ardhi hiyo ni ya familia yake.

Mpalestina huyu mwenye umri wa miaka 73 alisema kwamba hati hii, iliyorithiwa kutoka kwa babu yake, ilihifadhiwa kutoka kizazi hadi kizazi katika sura ya plastiki yenye kingo zilizovunjika.

"Hii ni hati ya kipindi cha Uthmaniyya inayoonyesha kuwa babu yangu 'Abdulfettah Mansour alinunua ekari 60 za ardhi huko Jurish. Hati hiyo inathibitisha kwamba ardhi ilinunuliwa na 'Abdulfettah Mansour.

Pia kuna muhuri wa Ottoman chini. Ardhi hii inamilikiwa na familia yetu tangu 1906." Picha ya mkulima wa Kipalestina huko Jurish akiwa ameshikilia hati ya mauzo ya miaka 117 iliyo na mhuri wa Ottoman inayothibitisha kwamba ardhi hiyo ni ya familia yake. 

Ottoman, mtawala wa kibabe wa maeneo mengi barani Ulaya, Asia na Afrika, aliitawala Mashariki ya Kati tangu karne ya 14, ikijulikana ka Boma ya Ottoman (Ottoman Empire). Utawala wake ulianza kufifia mwishoni mwa karne ya 17 na mwanzoni mwa 18, hasa baada ya kifo cha kiongozi wake, Suleiman the Magnificent


 

No comments