WATOTO 12 WA KATA MOJA WAFARIKI MKOANO KATAVI
Watoto 12 wa Kata moja wamefariki dunia ndani ya muda mfupi kufuatia mlipuko wa Ugonjwa wa Surua, uliotokea katika Kata ya Majimoto, mkoani Katavi.
Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Mpimbwe, Wilaya ya Mlele, Dkt. Martin Lohay, alithibitisha kutokea kwa vifo hivuo, akisema ugonjwa huo uliripotiwa tangu Februari 12, umewadhuru watoto hao walio chini ya umri wa miaka mitano.
Mganga huyo alisema licha ya vifo hivyo, uchunguzi umegundua uwepo wa watoto wengine 646 walioambukizwa na akatoa wito kwa wazazi kujenga mazoea ya kuwapeleka watoto kliniki mara kwa mara.

Post a Comment