JK, CONDOREECE, BILL GATES ANA KWA ANA WASHINGTON LEO
Rais Mstaafu wa awamu ya nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete leo atakuwa miongoni mwa wageni mashuhuri katika kuadhimisha miaka 20 ya mpango maalum wa kupambana na Ukimwi, PEPFAR, unaofanyika jijini Washington nchini Marekani.
Wageni wengine ni pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje wa zamani wa kwanza mweusi wa Marekani, Condoleeza Rice na tajiri namba moja duniani, Bill Gates.
Pia atakuwepo mwanzilishi wa mpango huo, Rais wa zamani wa Marekani George W Bush. Tukio hilo litafanyika katika Taasisi ya Amani ya Marekani na Rice anatarajiwa kuongoza mjadala wa kuchambua mafanikio, changamoto na maendeleo ya mpango huo duniani.

Post a Comment