WANAWAKE, VIJANA NA WALEMAVU KUKOPESHWA BILIONI 67.6

 MHE. UMMY MWALIMU AKITANGAZA NAFASI ZA AJIRA. - YouTube

 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Ummy Mwalimu amesema Serikali inayoongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan kupitia Mamlaka za Serikali za Mitaa imepanga kutoa shilingi Bil. 67.6 kama
Mikopo kwa Vikundi vya Wanawake, Vijana na Watu Wenye Ulemavu kwa mwaka wa fedha 2021/22.

Waziri Ummy ametoa kauli hiyo mapema leo Jijini Dodoma wakati akikabidhi hundi ya shilingi 1,039,050,000 kwa vikundi 48 vya Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Akikabidhi hundi hiyo Waziri Ummy amesema ni jukumu la kila halmashauri kuhakikisha katika makusanyo yake ya ndani inatoa asilimia 10 kwa ajili ya mikopo ya wanawake, vijana na walemavu.

Pia Waziri Ummy amezitaka Halmashauri kutumia wataalam wake kutoa elimu kwa vikundi vinavyotaka kukopo jinsi ya kutumia fedha hizo kwa miradi yenye tija na kuwaelimisha juu ya umuhimu wa kurejesha haraka ili na wengine waweze kunufaika.

Kwa upande wa mnufaika wa mikopo Bi.Gladius Jalee kutoka kikundi cha Jeshi Kubwa kilichopo Halmashauri ya Jiji la Dodoma ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita kwa kutekeleza azma ya kuendelea kusimamia na upatikanaji wa fedha za mikopo kwa kueleza kuwa kundi lao mpaka sasa wamefikia hatua zuri ya ukopeshwaji kutokana na urejeshaji wao mzuri kuanzia kukopeshwa kutoka shilingi milioni moja mpaka sasa kufikia kukopeshwa shilingi milioni hamisini.

No comments