NILIBONYEZWA MWILI MZIMA KUSAKWA MADAWA YA KULEVYA

 Kettering drugs overdoses linked to hazardous substance - BBC News

FLORENCE Khambi, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa Za Kulevya amesema kuwa aliposafiri kuelekea nchini China, mamlaka za huko walimsachi kwa kiwango cha juu, ikiwa ni pamoja na kubonyezwa kila sehemu ya mwili wake ili kusaka madawa ya kulevya akidhaniwa ameyabeba.

Kamishna huyo amesema Watanzania wanatajwa kuwa wanajihusisha zaidi na usafirishaji wa biashara ya dawa za kulevya (Mapunda/Punda) hasa katika nchi za China, Hong Kong na Afrika Kusini.

Amesema kuwa alipata wakati mgumu wakati aliposafiri kuelekea nchini China. Alifanyiwa ukaguzi wa hali ya juu sana.

"Nakumbuka wakati nilivyosafiri kwenda China kikazi nilifanyiwa ukaguzi usio wa kawaida. Nilipekuliwa sana nilibonyezwa sana mwili mzima"

No comments