AZIM DEWJI ANUNUA JEZI ZA MILIONI 20 NA KUZIGAWA KWA MASHABIKI WA TAIFA STARS

 Manara alipaswa kufikiria mbali zaidi ya Yanga"- Dewji | Picha

MFADHILI wa zamani wa Klabu ya Simba, Azim Dewji amesema ameamua kutumia Tsh. milioni 20 kununua Tshirt atakazozigawa kwa Vijana 2000 watakaoishabikia Timu ya Taifa ya Tanzania vs DRC Congo katika mchezo wa kuwania kufuzu fainali za kombe la Dunia.

Dewji ameyasema hayo leo na kuwataka Watanzania na Wadau wa soka kushirikiana kwa pamoja kuiunga mkono Taifa Stars katika mchezo huo utakaochezwa Novemba 11, 2021 na kuongeza kuwa atazikabidhi jezi hizo kwa TFF ambapo watazigawa kwa vijana hao 2000 ambao wataenda uwanjani kushabikia, pia atatoa tiketi 100 kwa ajili ya Wafanyakazi wake kwenda uwanjani.

"Tubadilike hii ni Timu yetu hatuombi pesa maana Waziri Mkuu ameshakusanya pesa na amepata za kutosha na Mama naye amesema ana imani na Timu, tumebakia sisi Wapenzi na Mashabiki kwamba lazima na sisi tuige na tufate yale yaliyozungumzwa na Viongozi wetu, tunaomba siku ya alhamis tuwape ruhusa Watanzania wakaishabikie Timu yetu"

No comments