TPA WATAKIWA KUJIPANGA KUFANYA BIASHARA
WAZIRI
wa Ujenzi na Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa ameitaka Mamlaka ya Bandari nchini kujipanga
kufanya biashara ili kukidhi malengo ya Serikali ya kutumia lango la bandari kukuza
uchumi wa nchi na wakazi wake.
Amesema
Serikali inatumia fedha nyingi kujenga na kukarabati miundombinu ya bandari hivyo
ni wakati sasa kwa watendaji na watumishi wa bandari kuleta biashara kubwa nchini
itakayoleta faida na kuhuisha uchumi wa sekta nyingine.
“Ni
wakati wa idara ya masoko ya bandari na watumishi wake kufanya kazi kimkakati wakilenga
kufanya biashara nakuzalisha faida”, amesema Prof. Mbarawa.
Amezungumzia
umuhimu wa watendaji wa bandari kuweka wahitimu wa fani za uhandisi katika miradi
ya ujenzi inayoendelea ili kuwajengea watanzania uwezo.
Zaidi
ya shilingi bilioni 440 zitatumika katika ukarabati mkubwa wa bandari ya Tanga na
kukamilika huko kutawezesha meli nyingi na kubwa kutumia bandari hiyo na kufufua
uchumi wa mkoa huo.
Amezungumzia
umuhimu wa uadilifu, ubunifu na uzalendo kwa watumishi wa bandari ili waweze kushindana
na bandari nyingine na kupata tija.
Naye
Mkuu wa Mkoa wa Tanga Adam Malima amemhakikishia Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi kuwa
mkoa huo utahakikisha unaweka mazingira salama na rafiki kwa wakandarasi wanaojenga miundombinu mkoani humo ili kufikia malengo ya kimkakati ya mkoa
na taifa kwa ujumla.
Prof. Mbarawa alikuwa katika ziara ya siku tatu mkoani
Tanga kukagua maendeleo ya
ujenzi wa miundombinu ya barabara, reli, vivuko, uwanja wa ndege na bandari.
IMETOLEWA NA KITENGO CHA HABARI
NA MAWASILIANO SERIKALINI WIZARA YA UJENZI NA UCHUKUZI

Post a Comment