TONY KARAMA WA SIKINDE AFARIKI GHAFLA

 Inaweza kuwa picha ya Mtu 1, ndani na maandishi

Mpiga bass maarufu wa Orchestra Mlimani Park "Sikinde Ngoma ya Ukae", Toni Karama amefariki ghafla muda mfupi ulipita.

Mrisho ambaye ni mtoto wa marehemu ameithibitishia Saluti5 kuwa Tony Karama amefariki dunia katika hospital ya Regency alipokimbizwa baada ya kuzidiwa ghafla.

Kwa sasa mwili wa marehemu umeshaenda kuhifadhiwa hospital ya Muhimbili na msiba uko Kariakoo mtaa Mafia na Jangwani.

Mrisho ambaye anapatikana kwa namba 0656802070 amesema taratibu za mazishi zitatangazwa muda mfupi ujao.

Onyesho la mwisho la Tony kushiriki na bendi yake ilikuwa Jumapili iliyopita katika ukumbi wa Loving Tone, Temeke.

Tony alirejea nchini wiki chache zilizopita akitokea Uturuki alipokwenda kushiriki matamasha ya muziki wa kiasili.

Credit: Salute 5

No comments