BIASHARA UNITED WAMTUMIA SALAMU ALLY HAPI KIAINA

UONGOZI wa Biashara
United umeweka wazi kuwa kwa sasa vichwa vinawauma kuhusu suala la usafiri wa
wachezaji wao kuelekea nchini Libya kwa ajili ya mchezo wa kimataifa wa Kombe
la Shirikisho dhidi ya Al Ahly Tripoli.
Biashara United inatoa
kilio hicho ikiwa kama ni salamu kiaina kwa Mkuu wa Mkoa wa Mara, Ally Hapi
ambaye aliwazawadia shilingi milioni kumi baada ya timu hiyo kuivimbia Simba na
kutoka nayo sare katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC.
Mchezo wa kwanza wa kusaka ushindi katika Kombe la Shirikisho raundi ya kwanza dhidi ya Al
Ahly Tripoli ya Libya utachezwa Oktoba 15, Uwanja wa Mkapa.
Seleman Mataso,
Mwenyekiti wa Biashara United amesema kuwa kuhusu mchezo wao wa nyumbani hawana
tatizo ila kinachowaumiza ni ule wa
marudio nchini Libya hali ni mbaya.
Mataso alibainisha kuwa
wanahitaji kufanya vizuri kimataifa ila hali ni tete kwenye upande wa mkwanja.
“Hali ni mbaya sana kwa
ajili ya mchezo wetu wa marudio ugenini, kwa muda huu gharama za matumizi ya safari mambo hayajakaa sawa na hata tiketi pia
bado hatujapata hivyo wadau watupe sapoti katika hili,” .
Biashara United
inayonolewa na Kocha Mkuu Patrick Odhhiambo iliweza kufika katika hatua hiyo
baada ya ushindi mbele ya Dikhil.Mchezo wa marudio
unatarajiwa kuchezwa Oktoba 23 nchini Libya.

Post a Comment