DIAMOND PLATNUMZ APEWA JEZI YA WASHINGTON NFL MAREKANI
NYOTA wa muziki wa kizazi kipya nchini,
Nasibu Abdul maarufu kama Diamond Platnumz, amepewa jezi namba 99 iliyoandikwa
jina lake na klabu ya Washngton NFL ambayo inashika nafasi ya Pili katika Ligi
Kuu ya Mpira wa Miguu wa Marekani( American Footbal).
Kupitia Ukurasa wao wa Instagram, timu hiyo imethibitisha
jambo hilo kwa kumposti msanii huyo ikiwa na ujumbe uliosomeka @diamondplatnumz repping the Burgundy & Gold - Washington NFL
Kwa sasa msanii huyo anaendelea na ziara yake ya kikazi nchini Marekani na
kesho atafanya onyesho Minnepolis na Ijumaa atakuwa Denver.

Post a Comment