BENARD MORISSON AWAKA KUTOITWA GHANA
MSHAMBULIAJI wa Kimataifa wa
Ghana na Klabu ya Simba, Bernard Morrison amelalamikia kitendo cha Kutoitwa
Kwenye Kikosi Cha timu ya Taifa ya Ghana 'Black Stars licha ya kucheza vizuri
akiwa na kilabu yake ya Simba SC.
Mshambuliaji huyo amelalamikia
kitendo cha kuitwa kwa nahodha wa Black Stars, Andre Ayew ambaye kwa sasa
anacheza soka huko Qatar kwenye nchi ambayo inachukuliwa na wengi kama sehemu
ambayo wanaenda kucheza wachezaji waliostaafu soka na huku yeye anayecheza soka
la ushindani zaidi yake ameachwa.
Morrison amesema akiitwa kwenye
kikosi cha Ghana anaweza kufanya vizuri zaidi kuliko wachezaji wanaocheza Qatar
lakini wanaitwa Black Stars na huku ikijulikana kabisa mchezaji pekee wa Qatar
katika Kikosi cha Black Stars ya sasa ni nahodha Andre Ayew,
"Ninaweza kufanya kazi
nzuri kuliko wavulana wengi wanaocheza Qatar. Kama unaweza kuwaita wachezaji
wanaocheza Ligi za Qatar, kwanini mimi nisiitwe ? ,Tunacheza mpira wa levo
moja, inaonekana ni aibu kwetu kucheza Afrika "
"Ndio maana nazikubali nchi
kama Zambia, Misri na Afrika Kusini kwa Sababu wanaita wachezaji wote
wanaostahili sio kwa kuangalia tu wale wanaocheza nje ya Afrika, kwa Black
Stars wanawaita wachezaji wanaocheza Ndani ya Afrika ambao ni Magolikipa tu
"
"Makocha waliopita walikuwa
wanawaita Wachezaji wanaocheza Ligi za Afrika na ndio maana waliweza kwenda
mbali zaidi, Hatuwahitaji hawa Makocha wa kigeni (Nje ya Afrika) ambao macho
yao huwa Ni kwa Wachezaji wanaocheza Ulaya tu "
" Ninaamini sisi
(tunaocheza Ndani ya Afrika) huwa tuna ari ya kulipambania Taifa Kuliko wao.
"

Post a Comment