POLEPOLE, GWAJI BOY, SILAA KIKAANGONI DODOMA LEO

HAMPREY Polepole, aliyekuwa mwiba kwa wana CCM enzi za
Uenyekiti wa Dkt John Pombe Magufuli akiwa Katibu wa Itikadi na Uenezi, leo
ataonja joto ya jiwe kibao kitakapomgeukia na kujikuta akiwa kikaangoni
akihojiwa na Kamati ya Maadili ya Wabunge wa CCM.
Wabunge wengine watakaohojiwa leo ni Askofu
Josephat Gwajima (Kawe) na Jerry Silaa (Ukonga) ambao Bunge lilipitisha azimio
la kuwasimamisha kwa mikutano miwili kutokana na tuhuma za kusema uongo,
kushusha hadhi na heshima ya Bunge.
Vilevile, Kamati imependekeza Askofu Gwajima
kufikishwa mbele ya kamati ya chama chake CCM na kuhojiwa kuhusu mwenendo wake.
Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge
ilipendekeza Silaa asimamishwe mikutano miwili ya Bunge la Tanzania na avuliwe
uwakilishi kwenye Bunge la Afrika (PAP) kwa madai kuwa anaweza kusema uongo
akienda huko.
Kilichomponza Silaa ni kauli yake ya kutaka
wabunge wakatwe kodi kwenye mapato yao, jambo lililoelezwa kuwa ni uongo, kwani
wabunge wanalipa kodi.
Kwa upande wa Gwajima, atatakiwa kujieleza kuhusu
kauli anazozitoa katika Kanisa lake la Ufufuo na Uzima kuanzia Julai 25 mpaka
Agosti 15 kuhusu chanjo ya korona.

Post a Comment